Kwa mujibu wa gazeti la Sabq, imearifiwa kuwa mashindano hayo yatasimamiwa na majaji wanne kutoka Saudia na sita kutoka nchi nyingine za Kiislamu.
Salman Ibn Mohammad Al Amri Mkuu wa Kamati ya Uhusiano wa Umma katika mashindano hayo amesema majaji Wasaudi katika mashindano hayo ni pamoja na Ibrahim ibn Sa’eed Aldsari, Emad ibn Zahir Hafez, Sheikh Sa’ud ibn Abdulaziz Alghanim na Salem Mahmoud Mahmoud Al-Shanqiti.
Majaji wa kimataifa katika mashindano hayo ni Ahmad Issa Hassan Al-Ma’sarawi kutoka Misri, Sheikh Samih Ahmad kutoka Jordan, Sheikh Mohammad Al-Mokhtar Al-Qasem Mohammad Al-Amin kutoka Mauritania, Sheikh Abdul Malek Abd Manaf Taher Lazem kutoka Malaysia, Taher Mohammad Rasul Hakim kutoka Pakistan na Shiekh Sadeq Sediq Zawiyah kutoka Nigeria .
Mashindano hayo yatafanyika katika mji mtakatifu wa Makka kuanzia 23-30 mwezi ujao wa Muharram. Kuna washiriki 161 kutoka nchi 53 duniani ambao watashiriki katika mashindano hayo ya qiraa na hifdhi ya Qur’ani Tukufu.
898584