IQNA

Kamati ya kuchapisha Msahafu wa Kitaifa Imarati yaundwa

16:57 - November 27, 2011
Habari ID: 2229963
Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Masuala ya Kiislamu ya Dubai amesema kuwa imeundwa tena kamati maalumu ya kuchapisha na kusambaza Msahafu wa Kitaifa wa Imarati kwa jina la Msahafu wa Sheikh Maktoum bin Rashid Aal Maktoum.
Hamad bin Sheikh Ahmad al Shaibani ametoa amri ya kuundwa kamati hiyo.
Wakati huo huo Abdur Rahim Muhammad Tahir Naibu Mwenyekiti wa mpango wa kuchapisha na kusambaza msahafu wa kitaifa wa Imarati amesema kuwa kuundwa kamati hiyo ni hatua muhimu katika njia ya kuchapisha msahafu wa kitaifa ambayo matunda yake yanaonekana siku baada ya siku.
Ameongeza kuwa kamati hiyo inafanya mashauriano na wataalamu na wakosoaji kwa ajili ya kuunda kundi la kusimamia uchapishaji wa msahafu huo. 906395

captcha