IQNA

Uchunguzi wa kutambua Uislamu, Qur’ani na Mtume Muhammad kufanyika Chuo Kikuu cha Missouri

23:52 - November 27, 2011
Habari ID: 2230061
Programu iliyopewa jina la ‘Lango la Amani: Utambuzi wa Uislamu, Qur’ani na Mtume Muhammad (saw) itafanyika tarehe 29 Novemba katika Chuo Kikuu cha Missouri nchini Marekani.
Programu hiyo imetayarishwa na Baraza la Uhusiano wa Kiislamu na Marekani (CAIR) kama jibu na kejeli iliyofanywa na mtu aliyejulikana kwa jina la Kamal Saliim dhidi ya Uislamu.
Mtu huyo ambaye kwa sasa ni Mkristo anatumia fursa yoyote anayopata kwa ajili ya kuuhujumu Uislamu.
Hivi karibuni Mmarekani huyo aliuhujumu Uislamu na Waislamu katika shughuli ya dua iliyofanyika Kansas City.
Baada ya mkasa huo Baraza la Uhusiano wa Kiislamu na Marekani lilichukua uamuzi wa kutayarisha ratiba hiyo ya kuwatambulisha watu mafundisho ya dini ya Kiislamu na Mtume Muhammad (saw). 905634
captcha