IQNA

Jumuiya ya Kulinda Qur'ani ya Jordan yashinda Tuzo ya Kimataifa ya Kuhudumia Qur'ani

16:16 - November 28, 2011
Habari ID: 2230751
Jumuiya ya Kulinda Qur'ani Tukufu ya Jordan imechaguliwa na Taasisi ya Kimataifa ya Kuhifadhi Qur'ani Tukufu kuwa mshindi wa Tuzo ya Kimataifa ya Kuhudumia Qur'ani Tukufu katika mwaka 2011.
Tuzo hiyo ya kimataifa imekabidhiwa na Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Uislamu Abdullah bin Abdul Muhsin al Turki katika sherehe zilizofanyika mjini Jiddah Saudi Arabia.
Jumuiya ya Kulinda Qur'ani ya Jordan imetunukiwa tuzo hiyo kutokana na kuwa na sifa kama kuwa na aina mbalimbali za shughuli za Qur'ani, nidhamu nzuri ya uendeshaji wa masuala ya kiidara, taathira kubwa za jumuiya hiyo, kutumia vyema suhula mbalimbali na kadhalika.
Ni vyema kukumbusha hapa kuwa Tuzo ya Kimataifa ya Kuhudumia Qur'ani Tukufu ilianzishwa mwaka 1426 Hijria kwa lengo la kuenzi vituo, taasisi na walimu hodari wa Qur'ani kwa shabaha ya kuzidisha motisha na moyo wa ushindani kati ya vituo vya elimu na mafunzo ya Qur'ani. 906980
captcha