IQNA

Chama cha Ikwanul Muslimin chaongoza katika uchaguzi Misri

13:29 - December 01, 2011
Habari ID: 2232433
Harakati ya Ikwanul Muslimin inaongoza katika uchaguzi wa kwanza wa bunge kufanyika baada ya mapinduzi nchini Misri.
Chama cha Uhuru na Uadilifu cha Ikwanul Muslimin kinaongoza katika matokeo ya awali ya duru ya kwanza ya uchaguzi wa bunge.
Mjini Cairo wafuasi wa Ikwanul Muslimin wamepata asilimia 47 ya kura zilizopigwa. Uchaguzi wa Baraza la Chini la Bunge la Misri utaendelea katika duru tatu kwa muda wa wiki sita.
Kuna wapiga kura milioni 40 nchini Misri na uchaguzi huu unatathminiwa kuwa hatua ya kwanza ya kuwaondoa madarakani watawala wa kijeshi na kuiweka madarakani serikali ya wananachi.
Uchaguzi huu ndio wa kwanza tokea mwamko wa Kiislamu wa wananchi umuangushe dikteta Husni Mubarak mwezi Februari. Harakati ya Ikwanul Muslimin ilipigwa marufuku wakati wa utawala wa Mubarak.908767
captcha