IQNA

Nakala nadra ya Qur'ani yavutia watazamani wengi Saudia

18:00 - December 03, 2011
Habari ID: 2233514
Maonyesho ya nakala ya Qur'ani Tukufu yenye umri wa miaka 300 yamewavutia watu wengi katika mji wa Jeddah nchini Saudi Arabia.
Nakala hiyo ya Qur'ani ambayo imepambwa kwa maji ya zafarani na wino wa Kichina, iliandikwa miaka 300 iliyopita na iliwavutua watazamani wengi katika maonyesho ya kimataifa ya mapambo ya nyumbani yaliyomaliza kazi zake jana mjini Jeddah.
Msimamizi wa maonyesho hayo Najlaa Falmban amesema kuwa bidhaa zilizoonyeshwa kwenye maonyesho hayo zimevutia watazamaji wengi lakini nakala hiyo ya Qur'ani ya kale ndio iliyotia fora kwa kuvutia idadi kubwa zaidi. 909406

captcha