Kapteni Mehdi Meydani amemwambia mwandishi wa IQNA kuwa mashindano hayo yataanza Jumatatu 19 Disemba katika makao makuu ya jeshi mjini Tehran.
Amesema washiriki ni kati ya walioshinda katika mashindano ya mchujo ya Qur'ani ya vikosi vya nchi kavu, anga, na wanamaji.
Kapteni Meydani ameongeza kuwa washiriki watashindana katika vitengo vya tarteel, hifdhi ya juzuu 3, 4, 5, 10, 20 na 25 pamoja na kuhifadhi Qur'ani kamili. Aidha kutakuwa na mashindano ya adhana.
Ameongeza kuwa washindi wa vitengo mbalimbali watatangazwa na kutunukiwa zawadi Jumatano Disemba 21.
912515