Qari huyo wa kimataifa amealikwa kushiriki katika mashindano ya Qur’ani yaliyoandaliwa na Jumuiya ya Qur’ani ya Sudan kati kati mwa mwezi Januari mwaka 2012.
Qari huyo wa Iran atashiriki katika mashindano hayo kupitia Shirika la Awqaf la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
Mohammad Mahdi Haqguyan ni qari mwenye umri wa miaka 14 na alianza kuhifadhi Qur’ani akiwa na umri wa miaka 8 na kufanikiwa kuhifadhi kikamilifu Qur’ani nzima baada ya miaka miwili.
924332