IQNA

Qari wa Iran kushiriki katika mashindano ya Qur’ani Sudan

16:51 - December 29, 2011
Habari ID: 2247491
Mohammad Mahdi Haqguyan, qari wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran atashiriiki katika mashindano ya kimataifa ya Qur’ani yatakayofanyika Sudan.
Qari huyo wa kimataifa amealikwa kushiriki katika mashindano ya Qur’ani yaliyoandaliwa na Jumuiya ya Qur’ani ya Sudan kati kati mwa mwezi Januari mwaka 2012.
Qari huyo wa Iran atashiriki katika mashindano hayo kupitia Shirika la Awqaf la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
Mohammad Mahdi Haqguyan ni qari mwenye umri wa miaka 14 na alianza kuhifadhi Qur’ani akiwa na umri wa miaka 8 na kufanikiwa kuhifadhi kikamilifu Qur’ani nzima baada ya miaka miwili.
924332
captcha