IQNA

Watalii laki tatu watembelea Nyumba ya Imam Khomeini

14:52 - December 31, 2011
Habari ID: 2248120
Zaidi ya watalii laki tatu wametembelea nyumba ya kihistoria ya Imam Khomeini Mwenyezi Mungu amrehemu katika mji wa Khomein katika mkoa wa Markazi kati mwa Iran.
Kwa mujibu wa Taasisi ya Kukusanya na Kuchapisha Athari za Imam Khomeini, takwimu zinaonyesha kuwa idadi ya watu waliotembelea nyumba hiyo kuanzia Machi mwaka 2011 imefika laki tatu.
Kwa mujibu wa ripoti hiyo watalii hao ni wa hapa nchini na kimataifa.
Ripoti hiyo imesema kuwa kuna programu kadhaa kwa ajili ya wageni wanaotembelea nyumba hiyo zikiwemo za kiutamaduni, maonyesho ya vitabu, kaligrafia, maonyesho ya nakshi n.k.
Mji wa Khomein ndiko alikozaliwa mwanzilishi wa Jmahuri ya Kiislamu ya Iran, Imam Ruhullah al Mousavi al Khomeini. Mji huo uko kati mwa Iran umbali wa kilomita 325 kutoka Tehran.
924636
captcha