Zaidi ya wawakilishi wa magazeti na majarida 27 kutoka mabara ya Asia, Afrika , Amerika na Ulaya wametangaza nia ya kushiriki katika kongamano hilo. Waandisha habari wanawake kutoka Iran pia watashiriki na wenzao wa kigeni. Kati ya nchi zilizotangaza kushiriki ni pamoja na Iraq, Tunisia, Misri, Russia , Bosnia na Herzegovina, Kosovo, Kazakhstan, Argentina na Thailand.
Kati ya malengo ya kongamano hilo ni kuarifisha majarida na magazeti ya wanawake Waislamu kutoka maeneo yote ya dunia. Aidha waandalizi wa kongamano hilo wana matumaini kuwa washiriki wataweza kuimarisha uwezo na ushirikiano wao ili kuinua kiwango cha vyombo vya habari vya Kiislamu. Kongamano hilo litaanza tarehe 7 mwezi huu wa Januari katika mji mkuu wa Iran, Tehran na kuendelea kwa siku saba.
926662