Taarifa iliyotolewa Baraza Kuu la Waislamu wa Uswisi imesema kuwa mkutano huo ambao ulipangwa kufanyika tarehe 25 Februari ukihudhuriwa na wanafikra 1800 wa Kiislamu kutoka maeneo mbalimbali duniani umefutwa kutokana na upinzani wa viongozi wa serikali za kieneo.
Taarifa hiyo imeongeza kuwa maafisa wa serikali wa miji miwili ya uswisi ambao awali walikuwa wameafikiana na maafisa wa Baraza Kuu la Waislamu wa Uswisi kuhusu jinsi ya kufanyika mkutano huo wametangaza kuwa hawatawapa Waislamu kumbi zilizotayarishwa kwa ajili ya kufanyika mkutano na kwa sababu hiyo wasimamizi wake wamelazimika kuufuta.
Baraza Kuu la Waislamu wa Uswisi ni moja ya taasisi kubwa zaidi za Kiislamu za nchi hiyo na linaongozwa na Nicolas Blancho. 955945