IQNA

Mashindano ya hifdhi na kiraa ya Qur'ani kufanyika Marekani

12:42 - February 20, 2012
Habari ID: 2276888
Mashindano ya hifdhi na kiraa ya Qur'ani Tukufu yamepangwa kufanyika tarehe 12 Mei huko Santa Clara katika jimbo la California nchini Marekani.
Kwa mujibu wa tovuti ya granadaschool, mashindano hayo huandaliwa kila mwaka na shule ya Kiislamu ya Granada kwa madhumuni ya kuwashawishi wanafunzi wajishughulishe zaidi na suala la kusoma na kuhifadhi kitabu hicho kitakatifu.
Mashindano hayo yatahusisha makundi manane ya wanafunzi wote wa shule za chekechea na za msingi.
Washiriki wa mashindano hayo wanaweza kushiriki katika kundi lolote la kuhifadhi sura zote zilizofundishwa katika shule hiyo katika kipindi cha mwaka mzima.
Waamuzi mashuhuri watatathmini juhudi za washiriki wa mashindano hayo na kisha kuwapa washindi zawadi kwa mujibu wa juhudi hizo. 956152
captcha