IQNA

Kongamano la 'Uislamu na Demokrasia' kufanyika Canada

21:05 - February 22, 2012
Habari ID: 2279185
Chuo Kikuu cha Ontario Magharibi nchini Canada kimeandaa kongamano la siku tatu lenye anwani ya 'Uislamu na Demokrasia'.
Kongamano hilo litafanyika Machi 23-25 mwaka huu kwa ushirikiano wa Chuo Kikuu cha Huron na Chuo Kikuu cha Kings Canada.
Kongamano hilo litachunguza muelekeo wa demokrasia katika nchi zenye Waislamu wengi duniani. Aidha washiriki watajadili mtazamo wa Uislamu kuhusu siasa. Mada zingine zitakazojadiliwa ni, 'Uislamu, Demokrasia na Nadhari ya Kisiasa, Uislamu, Demokrasia na Mfumo wa Katiba, Uislamu, Demokrasia na Siasa za Kisasa, Uislamu na Demokrasia na Utamaduni wa Kisiasa.
958379
captcha