Msemaji wa serikali ya Morocco Mustafa al Khulfi amesema kuwa Wizara ya Habari ya nci hiyo inataka kutekeleza mpango wa kukabiliana na propaganda chafu za kuwatisha watu kuhusu Uislamu na kuzuia maneno machafu dhidi ya Waislamu barani Ulaya kwa kushirikiana na Shirika la Elimu, Sayansi na Utamaduni la Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu.
Ameongeza kuwa wizara hiyo inashauriana na makampuni ya uchapishaji ya Ulaya katika uwanja huo kwa nia ya kuanzisha mapambano ya vyombo vya habari dhidi ya propaganda chafu zinazofanywa dhidi ya Uislamu.
Morocco haikutoa maelezo zaidi kuhusu mpango huo. 959654