Afisa wa kitengo cha habari cha Haram ya Imam Hussein (as) Alaa al Salami amesema kuwa masomo hayo ya kiraa ya Qur'ani Tukufu yalianza miezi minne iliyopita kwa lengo la kueneza utamaduni wa Qur'ani kati ya matabaka mbalimbali ya jamii ya Iraq.
Al Salami amemnukuu afisa anayeshughulikia masuala ya hifdhi ya Qur'ani katika Haram ya Hadhrat Abbas (as) akisema kuwa masomo hayo ya kiraa na tajwidi ya Qur'ani yanahusu kiraa, tajwidi na usahihishaji wa kiraa ya aya za Qur'ani.
Ametilia mkazo umuhimu wa masomo hayo na kusema lengo lake kuu ni kueneza sayansi ya Qur'ani, maarifa na utamaduni wa kitabu hicho kitakatifu katika jamii ya Iraq. 961611