IQNA

Jamii ya kimataifa yakosoa vikali ukiukwaji wa haki za binadamu Bahrain

17:35 - May 22, 2012
Habari ID: 2331874
Nchi zilizoshiriki katika kikao cha Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Matifa huko mjini Vienna Austria jana Jumatatu zilikosoa vikali ukiukwaji wa haki za binadamu nchini Bahrain unaofanywa na utawala wa nchi hiyo wa Aali Khali.
Wawakilishi wa Bahrain walioshiriki katika kikao hicho walishindwa kujibu majibu na lawama zilizotolewa dhidi ya watawala wa nchi hiyo kutokana na ukweli kwamba jinai na ukiukwaji wa haki za binadamu unaotekelezwa nchini humo dhidi ya raia wasio na hatia ni mkubwa mno kiasi kwamba hauwesi kutetewa wala kuhalalishwa kwa njia yoyote ile. Baraza hilo pia limewakosoa vikali watawala wa Bahrain kwa kutotekeleza mapendekezo yaliyotolewa na Kamati ya Kutafuta Ukweli iliyoongozwa na Mahmoud Sherif Bassiouni na pia kuongezeka kwa jela nchini humo. 1013972
captcha