IQNA

Mwanazuoni wa Kishia auawa kigaid nchini Nigeria

17:13 - May 29, 2012
Habari ID: 2337187
Ibrahim Sidi, mwanazuoni wa Kishia katika mji wa Potuskim katika jimbo la Yobe nchini Nigeria ameuawa kwa njia za kutatanisha hapo usiku wa Jumapili tarehe 27 Mei.
Mwanazuoni huyo aliuawa alipokuwa katika moja ya ofisi za Harakati ya Kiislamu jimboni humo. Mwanazuoni huyo ambaye ni ndugu yake Sheikh Mustafa Sidi alikuwa mwanachama muhimu wa jumuiya hiyo ya Kiislamu ambaye amekuwa akifanya harakati za kueneza mafundisho sahihi ya Uislamu wa Watu wa Nyumba ya Mtume Mtukufu (saw) katika mji huo. Pia amekuwa na rekodi ya kueneza mafundisho ya watukufu hao wa Kiislamu katika miji mingine ya Nigeria. Tukio hilo linajiri katika hali ambayo wiki mbili zilizopita wanaharakati wengine wa kidini waliuawa na watu wasiojulikana na ushahidi uliopo unaonyesha kuwa mauaji hayo yanatekelezwa kwa mpangilio maalumu. Hali hiyo imezusha hofu miongoni mwa Waislamu wa mji uliotajwa na kuongeza wasiwasi kuwa huenda wanaharakai wengine wa Kiislamu wakauawa katika siku zijazo kwa njia hiyohiyo ya kigaidi. Hadi sasa hakuna kundi lolote lililotangaza kuhusika na mauaji hayo na wala sababu za kutekelezwa kwake hazijulikani. 1019964
captcha