IQNA

Sayyid Nasrullah: Imam Khomein MA aliyaamsha mataifa ya Mashariki ya Kati

11:53 - June 02, 2012
Habari ID: 2339148
Katibu Mkuu wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Lebanon ya Hizbullah amesifu shakhsia adhimu ya Imam Khomeini MA na kusisitiza kwamba kiongozi huyo wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran alikuwa na nafasi muhimu na endelevu katika kuyaamsha mataifa ya eneo hili la Mashariki ya Kati na kaskazini mwa Afrika.
Sayyid Hassan Nasrullah amesema hayo katika hotuba yake kwa mnasaba wa kutimia miaka 23 tangu alipofariki dunia Imam Khomein MA Mwasisi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
Ameongeza kuwa, ana matumaini kuna siku umuhimu wa nafasi endelevu ya Imam Khomeini katika mabadiliko yote ya kieneo na hata mapinduzi ya nchi za Kiarabu, itajulikana zaidi.
Sayyid Nasrullah amemuelezea Imam Khomein kwamba alikuwa ni shakhsia adhimu, mwanafalsafa na mwanafikra mkubwa wa Kiislamu na kuongeza kwamba, Imam aliyekuwa na sifa za wazi na huku akielewa vyema umuhimu wa nchi kuwepo na uongozi na kiongozi, mara tu baada ya ushindi wa Mapinduzi ya Kiislamu alichukua hatua za kujenga na kuleta maendeleo nchini Iran.
1021696
captcha