Kwa mujibu wa televisheni ya al-Alam, magaidi hao walishambulia na kumuua Abdul Quddur Jabbara pamoja na ndugu yake karibu na haram takatifu ya Bibi Zeinab (as).
Hivi karibuni pia magaidi walilipua gari moja lililokuwa limetegwa bomu karibu na haram hiyo na kuwajeruhi watu wanne.
Wakati huohuo jeshi la Syria linaendeleza operesheni za kufagia magaidi katika mitaa tofauti ya mji wa Homs. Kuhusiana na suala hilo maafisa wa Syria wametangaza kuwa jeshi limefanikiwa kuusafisha mtaa wa Sultaniya kutokana na magenge hayo ya kigaidi. 1034026