Kwa mujibu wa gazeti la ad-Dastur linalochapishwa Misri, Hizbullah imetoa taarifa ikisema kuwa madai hayo yaliyotolewa na Wizara ya Fedha ya Marekani ni uongo mtupu usio na ukweli wowote.
Harakati hiyo vilevile imesisitiza katika taarifa yake kwamba uongo wa hivi karibuni uliotolewa na wizara iliyotajwa dhidi ya Hizbullah una lengo la kuiharibia jina harakati hiyo ya mapambano ya Kiislamu machoni pa walimwenguni.
Wizara ya Fedha ya Marekani imeituhumu Hizbullah kwamba inahusika na vitendo vya usafishaji pesa na ulanguzi wa madawa ya kulevya nchini Lebanon na Mashariki ya Kati! 1050364