Ugunduwaji wa kitabu hicho kitakatifu pamoja na maandishi mengine ya kihistoria ulifanywa siku ya Jumamosi na timu moja ya wataalamu wa mambo ya kale wa Chuo Kikuu cha Ataturk.
Qur'ani hiyo iliyogunduliwa ikiwa imefungwa kwenye kitambaa maalumu imepelekwa katika kitengo cha utafiti wa maandishi ya kihistoria yaliyoandikwa kwa mkono katika chuo kilichotajwa. Akizungumzia suala hilo, Dakta Huseyin Yurttas, mhadhiri wa masuala ya kihistoria katika Chuo Kikuu cha Ataturk na mkuu aliyesimamia timu ya uchimbaji katika ngome hiyo ya kale, amesema vitu vingine vilivyopatikana katika uchimbaji huo ni pamoja na nakala kadhaa za Qur'ani zlizoandikwa kwa maandishi ya dhahabu za karne za 18 na 19 na vilevile vitabu kadhaa vya fiqhi, itikadi na maudhui nyingine za Kiislamu. 1060165