Maafisa wa ofisi ya meya mjini humo wamedai kwamba wafanyakazi hao walifutwa kazi kwa kuwa hawangeweza kutekeleza vyema majukumu yao ya kuwahudumia watoto waliokuwa wakiwasimamia katika kambi ya mapumziko ya msimu wa joto wakiwa wamefunga.
Washiriki wa maandamano hayo wamesema wameandaa maandamano hayo kwa lengo la kutangaza mfungamano wao na wafanyakazi hao wa Kiislamu waliofutwa kazi kwa kutii amri ya dini yao. Wamesema lengo lao jingine ni kuwatangazia watawala wa Ufaransa kwamba saumu haikinzani kwa vyovyote vile na shughuli za kila siku.
Baadhi ya viongozi wa vyama vya kisiasa na kijamii vya nchi hiyo wamesema kwamba hatua ya meya ya kuwaachisha kazi wafanyakazi hao wa Kiislamu ilitokana na sababu za kisiasa.
Waislamu wa Ufaransa wamekuwa wakilalamikia vikali chuki na ubaguzi unaofanywa dhidi yao katika idara, shule, vyuo vikuu, mikahawa, kazini na maeneo ya umma nchini humo.
Kuzuiwa kuswali katika maeneo ya umma na pia kuvalia vazi la hijabu ni baadhi ya hatua ambazo zimechukuliwa na serikali ya Paris dhidi ya Waislamu wa nchi hiyo. 1071261