IQNA

Maandamano ya Quds yafanyika Ghaza

16:28 - August 18, 2012
Habari ID: 2395770
Maelfu ya wakazi wa Ukanda wa Gaza jana Ijumaa walifanya maandamano makubwa ya kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Quds ambapo walitangaza tena uungaji mkono wao kwa Quds Tukufu na Msikiti wa al-Aqsa.
Kwa mujibu wa tovuti ya Palestine Infor, washiriki wa maandamano hayo ambayo yaliandaliwa na wafuasi wa vyama vya kitaifa na Kiislamu walibeba mabango na bendera zilizokuwa na maandishi yanayounga mkono na kutetea matukufu ya Kiislamu na hasa Quds Tukufu.
Akizungumza katika maandamano hayo Rubah Mihna mmoja wa wanachama wa Chama cha Ukombozi wa Palestina PLO amesema ni muhali ukombozi wa Palestina kupatikana kupitia mazungumzo yasiyokuwa na maana na Wazayuni pamoja na waungaji mkono wao wa Magharibi.
Amemtaka Mahmoud Abbas, kiongozi wa Mamlaka ya Ndani ya Palestina asimamishe mara moja ushirikiano wake wa kiusalama na utawala ghasibu wa Israel na kushirikiana na Wapalestina wengine katika kupambana na jinai za utawala huo dhidi ya taifa la Palestina. 1081276
captcha