IQNA

Katibu Mkuu wa OIC:

Vitendo vinavyouhujumu Uislamu vipigwe marufuku

15:07 - September 30, 2012
Habari ID: 2423031
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu (OIC) ametaka kupigwa marufuku vitendo vya kuvunjiwa heshima Mtume Mtukufu wa Uislamu SAW.
Ekmeleddin Ihsanoglu amesema hayo katika radiamali yake dhidi ya filamu iliyotengenezwa na kusambazwa nchini Marekani inayomdhalilisha Mtume SAW.
Amesema Umoja wa Mataifa sambamba na kuheshimu matukufu ya dini na kuelewa masuala yanayopewa kipaumbele na ulimwengu wa Kiislamu, unapaswa kupasisha sheria zinazopiga marufuku kuvunjiwa heshima matukufu ya Kiislamu na kutangaza kwamba ni jinai kuuhujumu Uislamu.
Ihsanoglu amesisitiza kwamba, ubaguzi na vitendo vya utumiaji mabavu dhidi ya Waislamu vinatokana na uadui uliopo dhidi ya Uislamu na kwamba unakinzana na uhuru wa kusema ambao unadhaminiwa na sheria za kimataifa. 1109433
captcha