IQNA

Kubali cha kutangaza matangazo yaliyo dhidi ya Uislamu chatolewa Washington

21:17 - October 06, 2012
Habari ID: 2426447
Jaji mmoja wa mahakama ya serikali kuu ya Marekani mjini Washington DC jana Ijumaa alikiruhusu kikundi kimoja cha Wazayuni kilicho na misimamo ya kupindukia mipaka kuweka mabango yaliyo na matangazo ya chuki dhidi ya Uislamu katika vituo vya treni ya chini kwa chini mjini humo.
Kwa mujibu wa shirika la bahari la Associated Press, kibali kama hicho pia kilikuwa kimetolewa kwa kikundi hicho na mahakama nyingine mjini New York kuweka matangazo kama hayo kaika vituo vya treni ya metro au sub-way mjini humo.
Vitendo kama hivyo vilivyo dhidi ya matukufu ya Kiislamu vimeongezeka nchini Marekani baada ya filamu inayomvunjia heshima Mtume Mtukufu (saw) kutengenezwa nchini humo. 1113931
captcha