IQNA

Ripota wa UN:

Makampuni yanayojenga vitongoji vya walowezi Palestina yasusiwe

23:43 - October 26, 2012
Habari ID: 2437960
Ripota wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa katika ardhi zinazokaliwa kwa mabavu za Palestina amesema kuwa utawala wa Israel unazidi kupanua ujenzi wa vitongoji vya walowezi wa Kiyahudi katika ardhi za Palestina na ameitaka jamii ya kimataifa isusie na kuyawekea vikwazo makampuni yanayojishughulisha na ujenzi katika maeneo hayo.
Taarifa ya Richard Falk iliyowasilishwa jana katika Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa imesema makampuni kama Caterpillar, Hewlett Packard na Motorola ya Marekani, Veolia Environment la Ufaransa, G4S la Uingereza, Dexia la Ubelgiji na Volvo la Sweden ambayo yanafaidika na ujenzi wa vitongoji vya Wazayuni katika ardhi zinazokaliwa kwa mabavu za Palestina yanapaswa kuwekewa vikwazo vya kimataifa.
Amesisitiza kuwa ujenzi wa vitongoji hivyo haramu umeenea katika asilimia 40 na eneo la Ukingo wa Magharibi na ametoa wito wa kususiwa kimataifa makampuni hayo hadi pale yatakapoheshimu haki za binadamu na sheria za kimataifa. 1126372
captcha