IQNA imemnukuu Hamid Patel Mkuu wa shule ya Sekondari ya Wasichana ya 'Tawhidul Islam' akisema kuwa, wanafunzi Waislamu nchini Uingereza wanafanya vizuri kwenye masomo yao licha ya kukabiliwa na matatizo mengi. Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Tawhidul Islam iliyoko katika mji wa Blackburn pamoja na shule nyingine, zimeongoza kwenye orodha ya shule zilizofanya vizuri kimasomo katika mji huo. Takwimu zilizotolewa na Idara ya Elimu ya Uingereza inaonyesha kuwa, shule hiyo ndio bora zaidi nchini humo katika kuandaa mazingira ya mafanikio kwa mwanafunzi baada ya kutokuwa na kiwango kizuri kwenye shule ya msingi.
Mbali na shule ya Tawhidul Islam, zipo shule nyingine kadhaa za Kiislamu nchini Uingereza ambazo wanafunzi wake wamefanya vizuri na kuongoza kwenye taasisi za kielimu nchini humo. Inafaa kuashiria hapa kuwa, kuna karibu Waislamu milioni mbili na nusu nchini Uingereza na kwa mujibu wa takwimu za Baraza la Waislamu nchini humo kuna karibu wanafunzi laki nne ambao wanasoma katika shule mbalimbali. 1194144