IQNA

Rais-mteule wa Iran asisitiza msimamo wa wastani

16:40 - July 04, 2013
Habari ID: 2556326
Rais-mteule wa Iran Sheikh Hassan Rohani amesema kuwa msimamo wa wastani na busara ni mambo ambayo yataiwezesha Iran kukabiliana na matatizo ya kitaifa, kieneo na kimataifa.
Akizungumza mjini Tehran wakati alipokutana na maulamaa wa Iran, Sheikh Rohani amesema serikali inapaswa kutekeleza matakwa ya wananchi na kuhakikisha kuwa maisha yanaboreka.

Rohani amesema kuna haja ya kujiepusha na misimamo ya kufurutu mipaka na kuongeza kuwa, hivi sasa Iran inakabiliwa na matatizo makubwa ambayo hayajawahi kushuhudiwa katika historia.

Kuhusu uhusiano wa wananchi na maulamaa, Sheikh Rohani amesema maulamaa ndiyo ni sauti ya wananchi na ni kama daraja baina ya serikali ya wananchi.
Akiendelea na hotuba yake Sheikh Rohani ameashiria sehemu ya aya ya tisa ya Surat An-Nisaai katika Qur'ani Tukufu isemayo: 'Basi nao wamche Mwenyezi Mungu, na waseme maneno yaliyo sawa.' Amesema serikali na wanazuoni wanapaswa kuzingatia aya hiyo na kusema maneno yaliyo sawa wanapozungumza na wananchi.
1252168
captcha