IQNA

Maonyesho ya Kimataifa ya Qur'ani yaanza Tehran

16:59 - July 06, 2013
Habari ID: 2557152
Maonyesho ya 21 ya Kimataifa ya Qur'ani Tukufu yamefunguliwa leo mjini Tehran na Rais Mahmoud Ahmadinejad wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
Maonyesho hayo ya kimataifa yameanza alasiri ya leo katika uwanja mkubwa wa swala wa Imam Khomeoni.

Maonyesho ya Kimataifa ya Qur'ani mwaka huu yana vitengo 40 vikiwemo vya majarida ya Qur'ani, vyuo vikuu vya kidini na visivyo vya kidini, tarjumi ya Qur'ani Tukufu, Qur'ani, Vijana na watoto, mwenendo wa maisha ya Kiqur'ani, Qur'ani na dini mbalimbali, Qur'ani na sayansi, Qur'ani na umoja wa Kiislamu na kadhalika.

Maonyesho ya 21 ya Kimataifa ya Qur'ani Tukufu yataendelea hadi wiki ya mwisho ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhani
1252920
captcha