IQNA

Ban aulaani utawala ghasibu wa Israel kwa kujenga vitongoji

19:39 - February 01, 2016
Habari ID: 3470105
Katika makala aliyoiandikia gazeti la New York Times Jumatatu, Ban amesema ameulaani utawala harmau wa Israel kwa kujenga vitongoji vya Wazayuni katika ardhi za Palestina.

Katika makala aliyoiandikia gazeti la New York Times Jumatatu, Ban amesema ,"Historia imethibitisha kuwa watu daima watapambana dhidi ya kukaliw akwa mabavu ardhi zao."
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amelaani pia mpango wa Israel wa kujenga vitongoji vipya na kunyakua ekari 370 za ardhi za kilimo za Palestina katika eneo inalolikalia kwa mabavu la Ukingo wa Magharibi.
Amesema kupuuza dhulma ambazo Israel inawatendea Wapalestina hakuwezi kupelekea tatizo hilo kutoweka.
Katika siku za hivi karibuni, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amebainisha upinzani wake mkali kuhusu sera za Israel. Mnamo Janauri 26, akihutubu katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, Ban alisema Israel inapaswa kusitisha ujenzi wa vitongoji vya walowezi wa Kizayuni ili kupigwe hatua kuelekea amani. Siku iliyofuata, Ban alihutubua katika Kamati ya Umoja wa Mataifa kuhusu haki za Wapalestina na kusema, Wapalestina, hasa vijana wanapoteza matumaini na wamekasirishwa na sera za ukandamizaji wa utawala ghasibu wa Israel. Kauli hiyo ilipelekea waziri mkuu wa utawala wa Kizayuni kusema kuwa Umoja wa Mataifa unapendelea upande moja. Katika kujibu matamshi hayo ya Netanyahu, Ban ameandika makala katika gazeti la New York Times chini ya anuani ya: "Israel, mjumbe hauawi."
Zaidi ya Waisraeli nusu milioni wanaishi katika vitongoji 230 haramu vilivyojengwa katika ardhi za Palestina zilizoghusubiwa mwaka 1967 katika Ukingo wa Magharibi na Quds Mashariki.

3472027

captcha