
Kwa
mujibu wa mwandishi wa IQNA, Kongamano hilo limeandaliwa na Shirika la Elimu, Sayansi na Utamaduni la Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu (
ISESCO imetoa taarifa na kusema kuwa: "Kongamano hili limefanyika kwa lengo la kuimarisha na kustawisha ujuzi wa Huffadh wa Qur'ani sambamba na kuwapa mbinu mpya za kufundisha kuhifadhi Qur'ani Tukufu na kuwahimiza vijana na watoto kuhifadhi Qur'ani Tukufu."
Taarifa hiyo imesema: "Kongamano hili limeandaliwa kuwasilisha matokeo ya utafiti na uchunguzi katitka uga wa kustawisha taasisi na vituo vya Qur'ani ili kuhudumia kitabu cha Mwenyezi Mungu kwa njia inayostahiki. Aidha kongamano hili linalenga kuimarisha uhusiano baina ya wataalamu katika uga wa kufundisha kuhifadhi Qur'ani ili waweze kubadilishana uzoefu wao wa kikazi."