IQNA

Shakhsia 70 wa Qur'ani waenziwa Iran

11:52 - February 13, 2016
Habari ID: 3470133
Kongamano la 10 la Kuwaenzi Shakhsia wa Qur'ani Iran limefanyika Ijumaa usiku mjini Tehran.
Kikao hicho kimeudhuriwa na maafisa wa ngazi za juu wa masuala ya utamaduni na Qur'ani akiwemo Mkuu wa Shirika la Kuutangaza Uislamu Hujjatul Islam Seyyed Mehdi Khamoushi na Mkuu wa Shirika la Darul Qur'ani Mehdi Qarasheikhlu pamoja shakhsia wengine wa Qur'ani nchini.

Kikao hicho kilianza kwa qiraa ya Qur'ani Tukufu ya Qari Ustadh Abbas Salimu na kufuatia na hotuba ya Qarasheikhli ambaye alitoa ripoti fupi kuhusu kongamano hilo.

Katika hotuba yake aliwakumbuka quraa wa Qur'ani Tukufu kutoka Iran ambao waliaga dunia katika maafa ya Mina wakati wa msimu wa Hija nchini Saudi Arabia mwaka jana.

Akihutubu katika kikao hicho, Hujjatul Islam Khamousi alisisitiza ulazima wa kufahamu na kustawisha Qur'ani Tukufu.

Kati ya walioenziwa katika kikao hicho ni wanaharakati wa Qur'ani wakongwe, washindi wa mashindani ya kitaifa na kimataifa ya Qur'ani pamoja na waalimu mashuhuri wa Qur'ani.


Shakhsia 70 wa Qur'ani waenziwa Iran Shakhsia 70 wa Qur'ani waenziwa Iran

Shakhsia 70 wa Qur'ani waenziwa Iran

3474737

captcha