IQNA

Wananchi wa Bahrain waazimia kuendeleza mapambano dhidi ya utawala wa Aal Khalifa

9:10 - February 14, 2016
Habari ID: 3470137
Wananchi wa Bahrain wamekithirisha maandamano dhidi ya utawala wa ukoo wa Aal Khalifa katika siku za maadhimisho ya kuanza mamko wa Kiislamu.
Wabahrain wameandamana katika maeneo mbali mbali ya nchi hiyo siku ya Ijumaa ambapo wamelaani jinai za utawala wa Aal Khalifa huku wakitaka kuachuliwa huru wafungwa wa kisiasa na kupewa haki zao wananchi wa Bahrain.
Vikosi vya kijeshi Bahrain vimetumia gesi ya simu, mabomu ya sauti na risasi hai kuwatwanya wananchi waliokuwa wakiandamana kwa amani. Hivi sasa Bahrain iko katika hali ya hatari wakati wa kukaribia mmaadhimisho ya Mapinduzi ya wananchi. Ikumbukwe kuwa tokea Februari 14 mwaka 2011, wakati wa kuanza mapinduzi ya wananchi, takribani kila siku Bahrain imekuwa medani ya malalamiko na maandamano ya wananchi wanaotaka mabadiliko ya kisiasa.
Vikosi vya kijeshi vya Saudia na Imarati katika fremu ya 'Vikosi vya Ngao ya Peninsula' pamoja na askari wa nchi kadhaa za Kiarabu wako nchini Bahrain kuusaidia utawala dhalimu wa Aal Khalifa kukandamizwa wananchi. Hatua hiyo ya kukodi wanajeshi wa kigeni imewakasirisha sana wananchi wa Bahrain na hivyo kuzidisha hasira za wananchi dhdii ya utawala wa Aal Khalifa.
Matukio ya Bahrain yanaashiria kushika kasi mwamko wa wananchi wa Bahrain ambao wameazimia kuendeleza harakati za kimapiinduzi. Makundi ya kimapinduzi Bahrain yametangaza 'uasi wa kiraia' kwa mnasaba wa kuenzi siku ya kuanza mapinduzi ya wananchi. Mkaundi ya kimapinduzi Bahrain yamewataka wananchi kufunga maduka yao kuanzia Ijumaa Februari 12 Usiku hadi leo tarehe 14 Februari.
Makundi ya wanamapinduzi Bahrain pia yametaka wananchi wasitishe ushurukiano wao wa kibiashara na serikali pamoja na benki. Aidha wananchi wa Bahrain wametakiwa wasiende kazini, shuleni na vyui vikuu katika siku hizo tatu za uasi wa kiraia. Aidha wamenanchi wa Bahrain wametakiwa wasitii sheria za kidhalimu na wazuia kuingia mamluko wa utawala wa Aal Khalifa katika medani za maandamano. Ripoti zinasema wananchi wa Bahhrain wametii ombi hilo la uasi wa kiraia.
Matukio ya Bahrain ni ishara kuwa wananchi wangali wanaendeleza harakati ya kutetea haki zao.
Takwimu zinaoneysha kuwa maandamano dhidi ya serikali yalishahidi Bahrain mwaka 2015 na yameimarika zaidi katika mwaka huu wa 2016 na hayo yote ni ishara ya irada imara ya Wabahrain kufuatilia mwamko wao dhidi ya utawala wa kiimla wa Aal Khalifa ambao pamoja na kushahididisha ukandamizaji umeshindwa kuzima irada ya wananchi. Duru za kisiasa zinadokeza kuwa kushadidi maandamano ya Wabahrain katika wiki za hivi karibuni ni ishara ya kuimarika mwamako wa Wabahrain na ni pia dalili ya kufeli fikra za ubanaji na sera za kipolisi za utawala wa Aal Khalifa.
Duru mpya ya mwamko wa wananchi ni ishara kuwa pamoja na kuwepo ukandamizaji wa Aal Khalifa na tawala zinazounga mkono ukoo huo, wananchi wangali na uwezo na irada ya kuendeleza mwamko wao hadi pale yatakapojiri mabadiliko ya kimsingi katika nchi hiyo ndogo ya Ghuba ya Uajemi.
3459350
captcha