IQNA

Mafunzo kwa wanaohifadhi Qur'ani Tunisia

13:19 - March 01, 2016
Habari ID: 3470172
Waziri wa Masuala ya Kidini Tunisia imezindua mpango wa kutoa mafunzo kwa watu 100,000 waliohifadhi Qur'ani nchini humo.

Sheikh Mohammad Khalil amesema utekelezwaji mpango huo utaanzia katika jimbo la Nabeul na kuenea katika maeneo mengine ya nchi hiyo ya kaskazini mwa Afrika.

Amesema mkoa wa Nabeul umeteuliwa kuzinduliwa mpango huo kwa sababu ya historia yake ndefu ya harakati za Qur'ani.

Akizungumza akiwa huko Nabeul amebainisha matumaini yake kuwa mpango huo utaweza kuwafunza mahufadh laki moja wa Qur'ani. Aidha akiwa jimboni hapo ametembelea misikiti, vituo vya Qur'ani na jumuiya za Qur'ani.

Amesisitiza kuwa vituo kama hivyo vina nafasi muhimu katika kuwawezesha vijana kuhifadhi Qur'ani. Aidha amesesema wizara yake iko tayari kusaidia vituo hivyo katika kueneza utamaduni wa Qur'ani katika jamii ya Tunisia.

3479440

captcha