IQNA

Mashindano ya Qur'ani ya Amerika Kaskazini kufanyika California

13:03 - April 29, 2018
Habari ID: 3471487
TEHRAN (IQNA)- Mashindano ya Kusoma na Kuhifadhi Qur'ani ya eneo la Amerika Kaskazini yamepenga kufanyika wiki Ijayo nchini Marekani.

Kwa mujibu wa mwandishi wa IQNA awamu ya mchujo wa mashindano hayo itafanyika katika Kituo cha Kiislamu cha SABA ambapo wale watakaofika fainali watashindano katika Kituo cha Kiislamu cha Fatimya California Kaskazini. Mashindano hayo yanatazamiwa kufanyika baina ya Mei 5 hadi Mei 12.

Kituo cha Kiislamu cha SABA, katika mji wa San Jose, jimboni Califronia na kilifunguliwa katika muongo wa 80. Kituo hicho kuwa na harakati kadhaa za Kiislamu na kimeweza kufaunikiwa kuhudumia jamii ya Waislamu katika eneo hilo la Marekani.

3709955

captcha