IQNA

Narges Abyar apata zawadi ya 'Mwanamke Bora katika Ulimwengu wa Kiislamu'

17:19 - February 20, 2020
Habari ID: 3472489
TEHRAN (IQNA) – Mtengeneza filamu wa Iran Narges Abyar ametunukiwa zawadi kama 'mwanamke bora na aliyefanikiwa zaidi katika ulimwengu wa Kiislamu."

Bi. Abyar ametunukiwa zawai hiyo na Shirika la HUM la Pakistan ambalo hujishughulisha na masuala ya habari na lina baadhi ya televisehni kubwa zaidi katika nchi hiyo.

Abyar ameshinda zawadi kadhaa za kitaifa na kimataifa kutokana na kazi yake ya utegenejzaji filamu.  Zawadi ambayo Bi. Abyar ametunukiwa hutunukiwa wanawake ambao wameweza kupata mafanikio makubwa katika nchi mbali mbali duniani

Sherehe za kuwatunuku zawadi washindi wa mwaka huu zimefanyika katika mji wa Karachi Jumatano na kuhudhuriwa na Rais wa Pakistan Dkt. Arif Alvi na wageni wengin. Washindi wngine walikuwa ni Omer Aftab, Khadija Siddiqi, Dr Seemin Jamali, Dr Shamshad Akhtar, Jalila Haider, Maleeha Lodhi na Mary Robinson kutokana na kazi zao katika nyuga wanazojishughulisha nazo.

3880163

captcha