IQNA

Muislamu kuwa Kamanda wa Polisi Dearborn Marekani

21:37 - December 21, 2021
Habari ID: 3474702
TEHRAN (IQNA)- Issa Shahini ni Muislamu aliyehudumu kwa muda mrefu katika Idara ya Polisi ya Dearbon, jimboni Michigan Marekani na sasa ameteuliwa kuwa mkuu wa polisi katika mji huo.

Hayo yamedokezwa na Meya Mteule wa Michigan, Abdullah Hammoud ambaye amesema  kuanzia Januari Mosi Shahin atakuwa kamanda wa polisi katika mji huo na hivyo kumfanya kuwa Muislamu wa kwanza kushika wadhifa huo.  Shahin alianza kufanya kazi katika katika Idara ya Polisi ya Dearborn mwaka 1998.

Shahin pia ni mwanachama wa Jumuiya ya Kiislamu ya Amerika Kaskazini na Kamati Dhidi ya Ubaguzi ya Wamarekani- Waarabu.

Naye Hammoud ni Muislamu na Mwarabu-Mmarekani wa kwanza kuwa Meya wa Dearborn. Mji huo ni mashuhuri kwa idadi kubwa ya Waislamu na kwa muda sasa kumekuwa kukitolewa miito ya kutaka idara  za serikali ziakisi jamii ya watu wa Dearborn.

Mji wa Dearborn unakadiriwa kuwa na watu 110,000 na ni makao makuu ya shirika kubwa la Marekani la magari, Ford.

3477024

captcha