IQNA

Meya wa kwanza Muislamu Michigan aapishwa kwa Qur'ani

12:56 - January 16, 2022
Habari ID: 3474813
TEHRAN (IQNA)- Abdullah Hammoud ameapishwa kama meya wa kwanza Muislamu katika mji wa Dearborn jimboni Michigan ambapo amekula kiapo akiwa amewekelea mkono wake juu ya Qur'ani Tukufu.

Akihutubu baada ya kuapishwa, Hammoud alisema mji wa Dearborn  ni kielelezo cha utawala wa wananchi.

Hammoud ni Muislamu na Mwarabu-Mmarekani wa kwanza kuwa Meya wa Dearborn. Mji huo ni mashuhuri kwa idadi kubwa ya Waislamu na kwa muda sasa kumekuwa kukitolewa miito ya kutaka idara  za serikali ziakisi jamii ya watu wa Dearborn.

Mji wa Dearborn unakadiriwa kuwa na watu 110,000 na ni makao makuu ya shirika kubwa la Marekani la magari, Ford. Mji huo zamani ulikuwa mashuhuri kwa wabaguzi wa rangi kama vile Orville Hubbard ambaye alikuwa meya aliyetumia maneneo ya matusi dhidi ya Wamarekani Waafrika na Waarabu.

Katika sherehe za kuabishwa Hammoud, viongozi wa kidini wa Madhehebu za Kiislamu za Shia na Sunni pamoja na kasisi Mkristo waliongoza maombi kama njia ya kuonyesha umoja.

3477391

Kishikizo: deaborn michigan hammoud
captcha