Hayo yamedokezwa na mkuu wa jumuiya hiyo Sheikh Mohammad Hashad , ambaye amesema kwa mujibu wa uamuzi huo, yeyote ambaye anataka kujiunga na jumuiya hiyo anapaswa kuwa amehifadhi Qur'ani moyoni kikamilifu.
Amesema humuiya hiyo ina wanachama 9,000 na kwamba yeyote atakayekiuka kanuni atafikishwa katika kamati ya nidhamu.
Aidha ametoa wito kwa wasomaji Qur'ani kuhakikisha kuwa wanaposhiriki katika hafla ya mazishi hakuna msongamano wa watu.