IQNA

Maadili katika Qur'ani/ 26

Ukweli na Uaminifu; Vitu viwili vya Thamani Katika Maadili

19:35 - September 11, 2023
Habari ID: 3477580
TEHRAN (IQNA) – Ukweli na uaminifu ni vito viwili vya thamani ambavyo watu wanaweza kupata na kuchimba katika mgodi wa maadili kwa juhudi nyingi.

Tabia hizi mbili za kimaadili humsaidia mtu kufikia uongofu  katika ulimwengu huu na ujao, ni funguo za kugundua Undani  wa  watu (ubinafsi wa ndani) Kwa hiyo ikiwa unataka kujua kuhusu tabia nzuri na mbaya za mtu, unapaswa kuzijaribu kwa ukweli na uaminifu.

Tabia hizi mbili zina athari nyingi nzuri katika maisha ya mtu, Kwa mfano  wao husaidia kuongeza ufahari na heshima ya mtu miongoni mwa watu wengine, Ndio maana Imam Ali (AS) alihimiza kila mtu kuwa mkweli daima, kwa sababu mtu ambaye ni mkweli katika maneno yake, hadhi yake itakua katika jamii.

Ukweli pia humpa mtu ujasiri na ushujaa ambao kwa huo anaweza kupata amani ya akili, Uongo na unafiki, kwa upande mwingine, humfanya mtu kuwa na wasiwasi na woga kila wakati ili uwongo wake ufichuliwe na kupoteza heshima yake miongoni mwa watu.

Ukweli pia humfanya mtu kuwa thabiti katika kupinga madhambi na maovu, Kwa maneno mengine, inamsaidia kuepuka dhambi, anajua kuwa akifanya dhambi hawezi kuifunika, kwa hiyo anaepuka uovu na dhambi ili asije akajikuta katika hali hiyo.

Jinsi ya Kupata Baraka Zaidi za Mwenyezi Mungu

Ukweli na uwongo hudhihirika si kwa maneno tu bali pia kwa vitendo,wale ambao vitendo vyao ni kinyume cha wanavyohisi na kudhania ni waongo, Ndio maana wanafiki walipokwenda kwa Mtume Muhammad (S.A.W) na kushuhudia utume wake, iliteremshwa aya ya Qur’ani Tukufu ambayo ndani yake Mwenyezi Mungu anasema wanafiki wanasema uwongo, Muhammad (S.A.W) alikuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu na huu ndio ukweli lakini wanafiki wanaposhuhudia haya, wanasema uwongo kwa sababu sivyo wanavyoamini moyon mwao.

Ukweli ni wa thamani sana mbele ya Mwenyezi Mungu kiasi kwamba anasema katika  Tafsiri Aya ya 24 ya Surati Al-Ahzab; Hakika Mwenyezi Mungu atawalipa wakweli kwa ukweli wao na atawaadhibu au kuwasamehe wanaafiki apendavyo, Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusamehe na Mwenye kurehemu.

 

3485117

Kishikizo: ukweli Muhammad
captcha