Hii ni wakati mwanadamu kwa asili hana mwelekeo wa kufanya mabaya na kinachomfanya afanye ni vishawishi kutoka kwa Shetani, ambaye ameapa kumpoteza mwanadamu.
Shetani ni neno linalotumika kuita uovu wowote au mtu yeyote anayefanya uovu, Katika dhana za kidini, Shetani ni jina la mtu asiye wa kimwili ambaye wengine wanaamini kuwa ni malaika na wengine wanasema ni jini.
Kulingana na dini za Mwenyezi Mungu, kabla ya kuumbwa kwa Adamu, Shetani alikuwa mtumishi wa pekee wa Mwenyezi Mungu ambaye alimcha Mwenyezi Mungu sana na alikuwa na ujuzi mwingi mno, Hata hivyo, hakumtii Mwenyezi Mungu alipoamrishwa kumsujudia Adamu, Alifukuzwa peponi lakini akamuomba Mwenyezi Mungu ampe nafasi ya kuwapoteza wanadamu mpaka Siku ya Kiyama.
Tulipo waambia Malaika, Msujudieni Adam, wakamsujudia wote isipokuwa Iblisi Shetani aliyesema; Je, nimsujudie uliyemuumba kwa udongo? Alisema Kumbukeni haya ambaye umemtukuza kuliko mimi nitamleta yeye na dhuria wake wengi chini ya utawala wangu ikiwa utanipa muhula mpaka Siku ya Kiyama, Mwenyezi Mungu akasema; Ondoka, kwa atakayekufuata miongoni mwao, basi hakika Jahannamu ni malipo yako, ni malipo kamili, Tafsiri ya aya ya 61-63 ya Sura Al-Isra.
Majivuno ya Shetani na wazo lake kwamba alikuwa mkuu kuliko mwanadamu kwa sababu alikuwa anafanya ibada za Mwenyezi Mungu kwa muda mrefu vilimfanya amuasi Mwenyezi Mungu na kisha akawa adui wa mwanadamu aliyeapa, na kuapa kumpotosha vyovyote awezavyo, Akasema Shetani, Naapa kwa Uweza Wako, kwamba nitawapoteza wote , aya ya 82 ya Sura Saad.
Kinachowangojea Wanaopinga Dini
Kitu cha kwanza ambacho Shetani alifanya dhidi ya wanadamu kilikuwa ni kumpotosha Adamu (AS). Adamu (AS) na mke wake, Hawa, walioishi katika bustani walishawishiwa na Shetani kula tunda lililokatazwa na hilo likapelekea kufukuzwa kwao kutoka katika bustani hiyo.
Katika Qur’ani Tukufu, kuna marejeo 88 kwa Shetani, baadhi ya hayo yanahusu hadithi ya kuumbwa kwa mwanadamu, mengine kuhusu sifa za Shetani na wafuasi wake na hatima yao, na baadhi kuhusu jinsi Mitume wa Mwenyezi Mungu walivyokabiliana na vishawishi vya Shetani, Kusudi la marejeo haya ni kutusaidia kumjua Shetani na jinsi ya kukabiliana naye na majaribu yake.