IQNA – Chuo Kikuu cha Linnaeus kilichopo Växjö, Sweden, kimeripoti matukio mawili tofauti ya uharibifu wa Qur’an katika chumba chake cha swala kwenye jingo hilo.

Chuo hiki kiliarifu polisi wa eneo hilo kwamba majaribio ya kudhalilisha Qur’ani yalitokea wiki iliyopita. Katika matukio yote mawili, nyama ya nguruwe iliyowekwa chumvi iliwekwa ndani ya nakala kadhaa za kitabu kitukufu, kulingana na kituo cha habari cha ndani cha Alkompis.
Tukio la kwanza lilitokea Jumatano wakati vipande vya nguruwe vilipogunduliwa kwenye zulia la sala na ndani ya rafu za kuhifadhi Qur’ai Tukufu.
Siku iliyofuata, tukio la pili liliarifiwa, ambapo vipande vikubwa zaidi vya nguruwe viliwekwa juu na kati ya kurasa za Qur’ani.
Mwanafunzi mmoja aitwaye Ibrahim, ambaye alishuhudia matokeo ya tukio hilo la pili pamoja na mwanafunzi mwenzake, aliambia Alkompis kwamba walihisi harufu mbaya walipoingia katika chumba cha sala.
Walipokagua rafu za Qu’rani, walikuta vipande vya nguruwe ndani ya vitabu hivyo vitakatifu na mara moja waliripoti jambo hilo kwa maafisa wa chuo.
Katika kujibu, Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Linnaeus Peter Aronsson alilaani vikali matukio hayo katika taarifa rasmi, akisisitiza kujitolea kwa chuo hicho kwa kanuni za heshima na kutojumuisha ubaguzi.
"Tunalichukulia tukio hili kwa uzito mkubwa," Aronsson alisema katika taarifa iliyochapishwa kwenye tovuti ya chuo kikuu.
"Chuo kikuu kinasimamia heshima kwa thamani sawa na uhuru wa watu wote kama msingi wa kazi yetu. Hatutavumilia vitendo vyovyote vinavyokiuka haki za binadamu za wengine. Kuna uvumilivu wa sifuri kwa aina zote za ubaguzi katika chuo kikuu," alisema.
Tukio hilo limeripotiwa kwa polisi, alisema, na kuongeza kuwa chuo kikuu kimepanga hatua mbalimbali za usalama kusaidia wanafunzi wanaohisi wasiwasi kufuatia tukio hilo.
Sweden, katika miaka ya hivi karibuni, imekuwa kitovu cha kudhalilisha Waislamu. Mnamo mwaka 2023, Salwan Momika, Mkristo mzaliwa wa Iraq, alijulikana kwa kuchoma nakala za Qu’ani Tukufu hadharani wakati wa maandamano yaliyolindwa na polisi wa Sweden. Hivi karibuni aliuawa kwa kupigwa risasi katika nyumba yake ya Sweden.