“Natoa rambirambi zangu kwa msiba wa mke wako mtukufu, na naomba rehema na msamaha wa Mwenyezi Mungu kwa ajili yake,” alisema Ayatullah Khamenei katika ujumbe wake siku ya Jumatatu.
Rais wa Iran, Masoud Pezeshkian, Spika wa Bunge Mohammad Bagher Ghalibaf, pamoja na maulamaa wakuu na wasomi wa vyuo vya Kiislamu, akiwemo Ayatullah Abdullah Javadi Amoli, pia walitoa taarifa za rambirambi kufuatia msiba huo.
Mke wa Ayatullah Sistani alifariki Jumapili jioni baada ya kuugua kwa muda. Mazishi yake yalifanyika siku ya Jumatatu na mwili wake ukazikwa katika Msikiti wa Sheikh Tusi.
4307821