Jinai za Israel
TEHRAN (IQNA)- Kiongozi wa harakati ya Mapambano ya Kiisalmu (muqawama) ya Ansarullah ya Yemen amezitaka nchi za Kiarabu na Ulimwengu wa Kiislamu kuwa na misimamo ya wazi katika kukabiliana na mauaji ya kimbari yanayotekelezwa na utawala wa Israel dhidi ya Wapalestina katika Ukanda wa Gaza unaozingirwa.
Habari ID: 3477890 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/14
Jinai za Israel
LONDON (IQNA) - Askofu Mkuu wa Canterbury amesema hakuna msingi wowote wa kimaadili unaoweza kuhalalisha mauaji ya Wapalestina huko Gaza ambayo yanatekelezwa na utawala wa Israel.
Habari ID: 3477889 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/14
Jinai za Israel
AL-QUDS (IQNA) – Kitendo cha jinai cha Israel cha kulipua makao makuu ya Kamati ya Qatar ya Kujenga upya Gaza kimelaaniwa vikali na mataifa na jumuiya nyingi za Kiarabu na Kiislamu.
Habari ID: 3477888 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/14
Waungaji mkono Palestina
CAPE TOWN (IQNA) – Mji wa Cape Town nchini Afrika Kusini ulishuhudia maandamano makubwa zaidi katika jiji hilo katika miaka kadhaa wakati makumi ya maelfu ya watu walikusanyika kutangaza mshikamano na Palestina, wakitaka kukomeshwa kwa ukatili wa Israel huko Gaza.
Habari ID: 3477879 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/12
Jinai za Israel
GAZA (IQNA)- Kuendelea mashambulizi ya kila upande ya jeshi la Kizayuni dhidi ya Ukanda wa Gaza na kujiri mapigano makali kati ya vikosi vya muqawama na wavamizi hao karibu na kambi ya al-Shati iliyoko magharibi mwa mji wa Gaza, ni baadhi ya habari za hivi karibuni kutoka Palestina inayokaliwa kwa mabavu na utawala ghasibu wa Israel.
Habari ID: 3477873 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/10
Jinai za Israel
AL-QUDS (IQNA) – Utawala wa Kizayuni wa Israel hadi sasa umeshambulia na kuharibu kabisa kwa mabomu misikiti 56 tokea unazish vita vya maangamizi ya umati dhidi ya Ukanda wa Gaza. Aidha misikiti mingine zaidi ya 192 imepata hasara kwa kuharibiwa katika mashambulizi hayo ya kinyama.
Habari ID: 3477855 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/07
Kimbunga cha Al Aqsa
TEHRAN (IQNA)- Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina, Hamas, ameilaani vikali Marekani kutokana na uungaji mkono wake usio na masharti kwa kampeni ya kijeshi ya utawala haramu wa Israel dhidi ya Ukanda wa Ghaza. Aidha amesema utawala wa Israel umepata idhini ya Marekani ya kutekeleza mashambulizi dhidi ya Wapalestina katika Ukanda wa Ghaza.
Habari ID: 3477842 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/05
Kimbunga cha Al Aqsa
Al-QUDS (IQNA) - Kiongozi mkuu wa zamani wa harakati ya Jihad Islami (Jihadi ya Kiislamu) ya Palestina amesisitiza kuhusu azma ya taifa la Palestina kutetea ardhi yao inayokaliwa kwa mabavu na utawala haramu wa Israel.
Habari ID: 3477837 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/04
Jinai za Israel
TEHRAN (IQNA)- Katibu Mkuu wa Harakati ya Hizbullah ya Lebanon amesema machaguo yote dhidi ya utawala haramu wa Israel yapo mezani, huku akiuasa utawala huo wa Kizayuni usitishe mara moja uvamizi na mashambulizi yake ya kinyama dhidi ya Wapalestina wa Ukanda wa Gaza.
Habari ID: 3477836 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/03
Jinai za Israel
TEHRAN (IQNA)- Ikiwa ni katika muendelezo wa mauaji ya raia yanayofanywa na utawala haramu wa Israel, ndege za kivita za utawala huo hivi karibuni zilishambulia kwa mabomu kambi ya wakimbizi ya Jabalia iliyoko kaskazini mwa Ukanda wa Gaza na kuua kwa umati zaidi ya raia mia moja wa Palestina na kujeruhi wengine zaidi ya mia tatu.
Habari ID: 3477833 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/03
Kadhia ya Palestina
TEHRAN (IQNA)- Akizungumza leo katika sala ya Ijumaa ya mjini Tehran, Hujjatul Islam wal Muslimeen Kazem Sediqi amesema kuwa leo mrengo wa mapambano ya Kiislamu ni mrengo wa kimataifa na kuongeza kwamba mrengo huo umabadilisha dunia.
Habari ID: 3477832 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/03
Kadhia ya Palestina
DOHA (IQNA) - Muungano wa Kimataifa wa Wanazuoni wa Kiislamu (IUMS) ulitoa fatwa siku ya Jumanne, ukizitaka nchi za Kiislamu kuingilia kati ili kuwaokoa watu wa Gaza kutokana na mauaji ya kimbari yanayotekelezwa na utawala haramu wa Israel.
Habari ID: 3477825 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/01
Jinai za Israel
TEHRAN (IQNA)- Wapalestina wasiopungua 400, wengi wao wakiwa ni wanawake na watoto, wamethibitishwa kuuawa na kujeruhiwa baada ya mashambulizi ya anga ya utawala katili wa Israel dhidi ya wakimbizi ya Jabaliya katika Ukanda wa Ghaza.
Habari ID: 3477823 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/01
Kadhia ya Palestina
LONDON (IQNA) - Wazayuni hawawakilishi Uyahudi na wanataka "kuwaangamiza" watu wa Palestina, kuhani mwenye makao yake nchini Uingereza anasema huku kukiwa na mashambulizi ya Utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Ukanda wa Gaza yakiwa yamesababisha vifo vya zaidi ya Wapalestina 7,000 wengi wakiwa ni wanawake, watoto na wazee.
Habari ID: 3477793 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/10/27
Taarifa Muhimu
TEHRAN (IQNA) –Wahadhiri 9,200 wa vyuo vikuu vya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran wamelaani vikali ukatili wa utawala dhalimu wa Israel katika eneo la Palestina lililozingirwa la Ukanda wa Gaza.
Habari ID: 3477783 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/10/24
AL-QUDS (IQNA) - Israel ilizuia makumi ya maelfu ya Wapalestina kuingia katika Msikiti wa Al-Aqsa kwa siku ya Ijumaa ya 2 mfululizo.
Habari ID: 3477775 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/10/22
Milad un Nabii
AL-QUDS (IQNA) - Wapalestina waliadhimisha Maulidi yaani kumbukumbu ya kuzaliwa Mtume Muhammad (SAW) huko Al-Khalil na hasa katikak Msikiti Ibrahim huku kukiwa na vikwazo vikali vilivyowekwa na utawala haramu wa Israel ambao unaongoza kampeni ya kupinga Maulidi.
Habari ID: 3477668 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/09/29
Jinai za Israel
AL-QUDS (IQNA) - Vikosi vya utawala katili wa Israel siku ya Jumatano viliwashambulia Wapalestina, wakiwemo wanawake na watoto, ambao walikuwa wakiadhimisha siku ya kuzaliwa Mtume Muhammad (SAW) huko Al Quds (Jerusalem) Mashariki. Mji huo mtakatifu unakaliwa kwa mabavu na utawala haramu wa Israel.
Habari ID: 3477664 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/09/28
Watetezi wa Quds Tukufu
TEHRAN (IQNA)- Wanafunzi wa vyuo vikuu vya Mauritania wameandamana katika mji mkuu wa nchi hiyo Nouakchott, wakilaani kuanzishwa uhusiano wa kidiplomasia kati ya Waarabu na utawala haramu wa Kizayuni wa Israel.
Habari ID: 3477643 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/09/23
Kadhia ya Palestina
AL-QUDS (IQNA) - Msikiti wa Al-Aqsa katika mji wa al-Quds (Jerusalem) ni mahali pa ibada kwa Waislamu peke yao na ni haki takatifu isiyopingika kwao, mkuu wa Kamati ya Juu ya Rais ya Masuala ya Kanisa huko Palestina alisema.
Habari ID: 3477628 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/09/20