israel - Ukurasa 15

IQNA

Watetezi wa Wapalestina
TEHRAN (IQNA)- Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema: kadhia za Gaza zimewadhihirishia walimwengu hakika nyingi zilizofichika, na moja wapo ya hakika hizo ni uungaji mkono wa viongozi wa nchi za Magharibi kwa ubaguzi wa rangi.
Habari ID: 3477916    Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/19

Watetezi wa Palestina
TEHRAN (IQNA)- Watu wa Iran ya Kiislamu jana Jumamosi walishiriki katika maandamano makubwa kote nchini kuwatetea watoto wanaoendelea kuuawa wa Palestina sambamba na kulaani "mauaji ya watoto wachanga", "uhalifu", "mauaji ya kimbari", "mauaji ya halaiki", "ugaidi", "uhalifu wa kivita" na "maafa ya binadamu" yanayoendelea katika Ukanda wa Gaza.
Habari ID: 3477915    Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/19

Jinai za Israel
AL-QUDS (IQNA) - Msikiti wa Jamia wa Omari, ambao ni moja ya misikiti mikongwe zaidi katika Jiji la Kale la Gaza, uliripotiwa kulengwa katika mashambulizi ya anga ya utawala katili wa Israel siku ya Alhamisi.
Habari ID: 3477910    Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/18

Jinai za Israel
GAZA (IQNA)- Utawala haramu wa Israel umeua shahidi zaidi ya Wapalestina 12,000, wakiwemo watoto wasiopungua 5,000 tokea uanzishe vita vya mauaji ya kimbari dhidi ya Ukanda wa Gaza mnamo Oktoba 7.
Habari ID: 3477908    Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/18

Diplomasia
TEHRAN (IQNA)- Uzembe wa Umoja wa Mataifa na hasa mkwamo katika Baraza la Usalama la umoja huo ambao una jukumu muhimu la kulinda amani na usalama wa kimataifa, kuhusu vita vya Gaza, jinai za kivita na mauaji ya kimbari ya Wapalestina yanayofanywa na utawala wa Kizayuni, umekosolewa vikali kimataifa.
Habari ID: 3477904    Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/17

Jinai za Israel Gaza
TEHRAN (IQNA)- Wataalam wa Umoja wa Mataifa wametoa wito kwa Jumuiya ya kimataifa kuzuia mauaji ya kimbari dhidi ya watu wa Palestina wa Gaza huku utawala katili wa Israel ukiendeleza vita vyake dhidi ya eneo hilo lililozingirwa.
Habari ID: 3477903    Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/17

Muqawama (Mapambano ya Kiislamu)
BEIRUT (IQNA)- Naibu Katibu Mkuu wa Hizbullah ya Lebanon ameongeza kuwa, "Kuhusu kuenea kwa vita, uwezekano huo upo, iwapo watatushambulia, tutalazimika kujihami na tutatumia nguvu zetu zote. Hatuogopi vitisho vya Israel, tunaamini kuwa tutashinda."
Habari ID: 3477901    Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/17

Kimbunga cha Al Aqsa
Israel WASHINGTON, DC (IQNA) - Asilimia 60 ya Waislamu nchini Marekani wanaunga mkono Operesheni ya Kimbunga cha Al-Aqsa ya Harakati ya Kiislamu ya Kupigania Ukombozi wa Palestina, Hamas, dhidi ya utawala wa Israel, wakisema kundi hilo la kupigania ukombozi lilikuwa na haki katika mashambulizi yake.
Habari ID: 3477896    Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/15

Jinai za Israel
TEHRAN (IQNA) - Kufuatia mauaji ya hivi sasa yanayofanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel katika Ukanda wa Gaza, hakutakuwa na nafasi kwa ulimwengu wa Kiislamu kutegemea mazungumzo ya makubaliano na utawala huo, mwanazuoni mmoja wa Kiislamu amesema.
Habari ID: 3477895    Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/15

Jinai za Israel
TEHRAN (IQNA)- Kiongozi wa harakati ya Mapambano ya Kiisalmu (muqawama) ya Ansarullah ya Yemen amezitaka nchi za Kiarabu na Ulimwengu wa Kiislamu kuwa na misimamo ya wazi katika kukabiliana na mauaji ya kimbari yanayotekelezwa na utawala wa Israel dhidi ya Wapalestina katika Ukanda wa Gaza unaozingirwa.
Habari ID: 3477890    Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/14

Jinai za Israel
LONDON (IQNA) - Askofu Mkuu wa Canterbury amesema hakuna msingi wowote wa kimaadili unaoweza kuhalalisha mauaji ya Wapalestina huko Gaza ambayo yanatekelezwa na utawala wa Israel.
Habari ID: 3477889    Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/14

Jinai za Israel
AL-QUDS (IQNA) – Kitendo cha jinai cha Israel cha kulipua makao makuu ya Kamati ya Qatar ya Kujenga upya Gaza kimelaaniwa vikali na mataifa na jumuiya nyingi za Kiarabu na Kiislamu.
Habari ID: 3477888    Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/14

Waungaji mkono Palestina
CAPE TOWN (IQNA) – Mji wa Cape Town nchini Afrika Kusini ulishuhudia maandamano makubwa zaidi katika jiji hilo katika miaka kadhaa wakati makumi ya maelfu ya watu walikusanyika kutangaza mshikamano na Palestina, wakitaka kukomeshwa kwa ukatili wa Israel huko Gaza.
Habari ID: 3477879    Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/12

Jinai za Israel
GAZA (IQNA)- Kuendelea mashambulizi ya kila upande ya jeshi la Kizayuni dhidi ya Ukanda wa Gaza na kujiri mapigano makali kati ya vikosi vya muqawama na wavamizi hao karibu na kambi ya al-Shati iliyoko magharibi mwa mji wa Gaza, ni baadhi ya habari za hivi karibuni kutoka Palestina inayokaliwa kwa mabavu na utawala ghasibu wa Israel.
Habari ID: 3477873    Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/10

Jinai za Israel
AL-QUDS (IQNA) – Utawala wa Kizayuni wa Israel hadi sasa umeshambulia na kuharibu kabisa kwa mabomu misikiti 56 tokea unazish vita vya maangamizi ya umati dhidi ya Ukanda wa Gaza. Aidha misikiti mingine zaidi ya 192 imepata hasara kwa kuharibiwa katika mashambulizi hayo ya kinyama.
Habari ID: 3477855    Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/07

Kimbunga cha Al Aqsa
TEHRAN (IQNA)- Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina, Hamas, ameilaani vikali Marekani kutokana na uungaji mkono wake usio na masharti kwa kampeni ya kijeshi ya utawala haramu wa Israel dhidi ya Ukanda wa Ghaza. Aidha amesema utawala wa Israel umepata idhini ya Marekani ya kutekeleza mashambulizi dhidi ya Wapalestina katika Ukanda wa Ghaza.
Habari ID: 3477842    Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/05

Kimbunga cha Al Aqsa
Al-QUDS (IQNA) - Kiongozi mkuu wa zamani wa harakati ya Jihad Islami (Jihadi ya Kiislamu) ya Palestina amesisitiza kuhusu azma ya taifa la Palestina kutetea ardhi yao inayokaliwa kwa mabavu na utawala haramu wa Israel.
Habari ID: 3477837    Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/04

Jinai za Israel
TEHRAN (IQNA)- Katibu Mkuu wa Harakati ya Hizbullah ya Lebanon amesema machaguo yote dhidi ya utawala haramu wa Israel yapo mezani, huku akiuasa utawala huo wa Kizayuni usitishe mara moja uvamizi na mashambulizi yake ya kinyama dhidi ya Wapalestina wa Ukanda wa Gaza.
Habari ID: 3477836    Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/03

Jinai za Israel
TEHRAN (IQNA)- Ikiwa ni katika muendelezo wa mauaji ya raia yanayofanywa na utawala haramu wa Israel, ndege za kivita za utawala huo hivi karibuni zilishambulia kwa mabomu kambi ya wakimbizi ya Jabalia iliyoko kaskazini mwa Ukanda wa Gaza na kuua kwa umati zaidi ya raia mia moja wa Palestina na kujeruhi wengine zaidi ya mia tatu.
Habari ID: 3477833    Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/03

Kadhia ya Palestina
TEHRAN (IQNA)- Akizungumza leo katika sala ya Ijumaa ya mjini Tehran, Hujjatul Islam wal Muslimeen Kazem Sediqi amesema kuwa leo mrengo wa mapambano ya Kiislamu ni mrengo wa kimataifa na kuongeza kwamba mrengo huo umabadilisha dunia.
Habari ID: 3477832    Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/03