IQNA

Thamani za Mapinduzi ya Kiislamu lazima zilindwe’

10:45 - January 11, 2014
Habari ID: 1353133
Khatibu wa sala ya Ijumaa mjini Tehran amesema kuwa, timu ya mazungumzo ya nyuklia ya Iran huko Geneva inapasa kuwa makini na kwamba inapasa kuendelea na mazungumzo hayo ya nyuklia na kundi la 5+1 katika kalibu ya kuhifadhiwa maslahi ya taifa la Iran.

Ayatullah Muhammad Ali Movahhedi Kermani ameongeza kuwa, timu ya mazungumzo ya nyuklia ya Iran inapasa kulipatia kipaumbele suala la kulindwa thamani za mapinduzi, izza na utukufu wa Kiislamu. Akieleza kwamba wananchi wa Iran wanataka mazungumzo yafanyike kwa uwazi kabisa, Ayatullah Kermani amesisitiza kuwa, timu ya mazungumzo ya Iran haipasi kulipatia kundi la 5+1 mwanya wa kuamua walitakalo. Ayatullah Kermani ameshangazwa na msimamo wa kiadui wa Marekani wa kuizuia Jamhuri ya Kiislamu ya Iran isishiriki kwenye mazungumzo ya Geneva 2 yanayojadili mgogoro wa Syria na kuongeza kuwa, siyo shani kabisa kwa nchi kubwa na yenye ushawishi  kama vile Iran isishiriki kwenye mazungumzo hayo. Akizungumzia harakati zinazodi kuongezeka za makundi ya kigaidi na yale yanayowakufurisha Waislamu wengine katika nchi za Kiislamu kama vile Iraq na Syria, Khatibu wa sala ya Ijumaa ya mjini Tehran amesisitiza kuwa wanachuoni na maulamaa wa ulimwengu wa Kiislamu na wapenda haki kote ulimwenguni  wana jukumu la kuzifichua njama za watenda jinai. Ayatullah Kermani amelaani mauaji wanayofanyiwa  Waislamu wa Madhehebu ya Shia katika baadhi ya nchi za Kiarabu kunatokana na propaganda chafu za watawala wa nchi hizo waliokuwa na chuki dhidi ya Mashia, na kuongeza kuwa jinai hizo  zinaonyesha wazi undumakuwili wa baadhi ya viongozi wa nchi za Kiarabu.

1352882

captcha