Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran aliyasema hayo Jumamosi tarehe 11 Januari mjini Tehran wakati alipokutana na Pat Breen, Mwenyekiti wa Kamati ya Sera za Kigeni na Biashara katika Bunge la Kitaifa la Ireland (Oireachtas). Zarif aliongeza kuwa uhusiano wa Iran na Ireland unaweza kuimarishwa hasa katika nyanja ya biashara. Zarif alisema safari za wabunge wa nchi za Ulaya Tehran ni ishara ya kuwa Magharibi inataka kuimarisha uhusiano na Jamhuri ya Kiislamu. Aliendelea kusema kuwa kuwa safari hizo zinaashiria irada ya pande zote mbili kuimarisha uhusiano.
Breen kwa upande wake amesema Ireland ina azma ya kuimarisha uhusiano wa kisiasa na kibiashara na Iran.
1357691