IQNA

Mufti wa Lebanon aonya kuhusu njama za Marekani

9:03 - January 29, 2014
Habari ID: 1367878
Sheikh Muhammad Rashid Qabbani Mufti wa Lebanon amesema kuwa, Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel zinazusha fitina katika nchi za Kiarabu ikiwemo Lebanon na kuongeza kwamba fitina hizo ni sehemu ya Mpango wa Mashariki ya Kati Mpya lakini mpango huo hautafaulu.

Sheikh Qabbani ameeleza kuwa, Israel inatumia hali hiyo kupanua vitongoji vya walowezi wa Kizayun, kuwahamisha Wayahudi kutoka maeneo tofauti duniani na kuwapeleka ardhi za Palestina zinazokalia kwa mabavu huku ikiwafukuza Wapalestina ambao ndio wamiliki asili wa ardhi hizo. Mufti wa Lebanon pia amekosoa operesheni za kigaidi za kujilipua kwa mabomu nchini Lebanon na Mashariki ya Kati, na kusisitiza kwamba kila mtu anayewaua watu bila hatia kwa kujilipua, basi atakuwa amefanya dhulma na dhambi kubwa.
1367360

captcha