Sheikh Qabbani ameeleza kuwa, Israel inatumia hali hiyo kupanua vitongoji vya walowezi wa Kizayun, kuwahamisha Wayahudi kutoka maeneo tofauti duniani na kuwapeleka ardhi za Palestina zinazokalia kwa mabavu huku ikiwafukuza Wapalestina ambao ndio wamiliki asili wa ardhi hizo. Mufti wa Lebanon pia amekosoa operesheni za kigaidi za kujilipua kwa mabomu nchini Lebanon na Mashariki ya Kati, na kusisitiza kwamba kila mtu anayewaua watu bila hatia kwa kujilipua, basi atakuwa amefanya dhulma na dhambi kubwa.
1367360