IQNA

Nchi za Magharibi zinatekeleza njama dhidi ya Iran

17:03 - November 29, 2008
Habari ID: 1713931
Hakuna siku ambayo nchi za Magharibi zimeridhia maendeleo ya nchi za Kiislamu na hivi sasa zinatekeleza njama kubwa dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ili kuifanya isifikie maendeleo na ustawi inaoukusudia.
Hayo yamesemwa na Barakat, muhadhiri wa masuala ya falsafa ya Kiislamu katika chuo kikuu cha Damascus nchini Syria. Ameyasema hayo katika siku ya pili ya kikao cha ‘fikra ya pamoja ya wanachuo wa Ulimwengu wa Kiislamu’ mjini Tehran. Huku akisisitiza kwamba umoja na mshikamano wa Waislamu utapelekea kufichuliwa na kushindwa kwa njama za Marekani dhidi ya Waislamu, Ustadh Barakat amesema kuwa, Waislamu wana wasiwasi mkubwa kuhusiana na kuenea satuwa na ushawishi wa Marekani katika nchi za Kiislamu kwa sababu jambo hilo bila shaka litagonganisha na kuwagawa Waislamu katika makundi tofauti hasimu. Ameashiria umuhimu wa kuwepo muamko wa Waislamu katika kukabiliana na njama za nchi za Magharibi dhidi ya Waislamu na kuongeza kuwa, umoja na mshikamano unapaswa kuimarishwa miongoni mwa Waislamu kupitia mazungumzo. Amesema, nchi za Ulaya zinaungana kwa ajili ya kulinda maslahi yao na kwamba, nchi za Kiislamu ambazo wananchi wao wana itikadi na imani inayofanana, zinapasa kuwa mstari wa mbele katika kuimarisha umoja miongoni mwa Waislamu na hatimaye kuungana. 326959

captcha