Kikao hicho kinasimamiwa na viongozi wa Vatican na Jumuiya ya Kimataifa ya Ulinganiaji wa Kiislamu.
Miongoni mwa maudhui muhimu za kikao hicho ni mjadala juu ya 'nyadhifa za kidini', 'nyadhifa za kijamii na kitamaduni' na 'mpango wa kuitisha vikao vya dini mbalimbali wakati wa migogoro'.
Kikao hicho kinafuatia kile cha mwezi uliopita mjini Vatican ambacho kilifanyika kwa shabaha ya kuimarisha maelewano na amani baina ya dini mbili kuu za Kiislamu na Kikristo.
Ni vyema kukumbusha hapa kuwa Waislamu wanaunda karibu jamii ya watu bilioni moja na nusu huku Wakristo wakiwa karibu bilioni mbili kote duniani. 334657